Tukio hilo la aibu na kusikitisha lilitokea Februari 29, mwaka huu, saa nane mchana ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar.
Awali, Fatuma alionekana akiwa ameketi na mashosti zake wakipata ofa ya pombe kutoka kwa mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Peter ambapo baada ya muda alitokea demu mwingine na kwenda kukaa meza nyingine.
Baada ya Fatuma ambaye muda mwingi alikuwa akijua kuwa ndiye atakayeondoka na Peter kwa madai ni mzuri kuliko wenzake kuhisi anataka kuachwa solemba, alinyanyuka na kwenda kumletea ‘vagi’ yule demu aliyewatibulia.
Maneno hayo yaliamsha hasira kwa Peter ambaye alinyanyuka na kuanza kumshushia kipigo Fatuma kiasi cha kuzua timbwili zito na kujaza watu.
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi huo, binti huyo alisema: “Mimi namshangaa sana yule kaka, kunipiga bila sababu za msingi, kama ni ofa sijamuomba, amenipa mwenyewe, kwa nini anipige?” alihoji Fatuma huku akiondoka eneo hilo akiwa amenyong’onyea.
No comments:
Post a Comment