Sunday, March 4, 2012

BINTI WA MIAKA 10 AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME

Image of Binti wa miaka 10 ajifungua mtoto wa kiume
Binti wa miaka 10 ajifungua mtoto wa kiume


Mtoto huyo, alizaliwa kwa kupitia upasuaji inayojulikana kama Caesarian Section katika Hospitali ya Wanawake katika mji wa Puebla na sasa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa pneumonia.

Msichana huyo anaendelea vizuri kiafya na amesharejea nyumbani baada ya kujifungua, na anamtembelea mtoto wake hospitali kila siku.

Mwendesha mashtaka wa mji wa Puebla anafanya uchunguzi kumtafuta mwanaume aliyefanya ngono na msichana huyo, sababu hiyo inachukuliwa kama ni ubakaji kutokana na umri wa binti huyo.

Hii si maraya kwanza kwa msichana mwenye umri mdogo sana kujifungua nchini Mexico.

Mwezi Agosti mwaka jana, msichana Amalia, aliyekuwa na umri wa miaka 11, alijifungua mtoto baada ya vyombo vya sheria kutomruhusu kutoa mimba (abortion) kutokana na sheria ya Mexico kutoruhusu utoaji mimba ikivuka miezi mitatu.

Amalia alipata mimba baada ya kubakwa mara kwa mara na baba yake wa kambo kuanzia wakati ana umri wa miaka 10.

HOUSEGIRL AWEKA DAMU KWENYE UJI WA MTOTO

Image of Housegirl mwenye HIV achakachua uji wa mtoto wa bosi na damu yake ya hedhi (period)
Housegirl mwenye HIV achakachua uji wa mtoto wa bosi na damu yake ya hedhi (period)Housegirl mwenye umri wa miaka 17 amebambwa akiweka damu yake ya hedhi (period) kwenye uji wa mtoto wa muajiri wake, mwenye umri wa miaka 4. Msichana huyo anayeitwa Pelagia Mureya, alifanya kioja hicho cha kutisha nchini Zimbabwe
kwa mujibu wa website ya NewsDay, Miss Mureya, ambaye ni HIV positive, alifanya kitendo hicho cha kikatili mara kadhaa kabla ya kukamatwa

Uchakachuaji huo uligundulika pale mwajiri wake aliona tone la damu wakati mtoto wake akila uji, na kufanya "uchunguzi."

Baada ya kukamatwa, Mureya alidai hafahamu damu imetoka wapi

Mwajiri wake alichukua uji, mtoto wake na mjakazi Hospitali Gutu Vijijini ambapo vipimo vilithibitisha ilikuwa ni damu ya hedhi ya Mureya.

Mureya, ambaye ni kutoka kijiji cha Chinhoyi, alihukumiwa miaka 10 jela.

Hakukuwa na maelezo yaliyotolewa ni kwa nini aliweka damu kwenye uji wa mtoto wa muajiri wake.

Saturday, March 3, 2012

REMEMBER MICHAEL

http://www.africapoint.net/wp-content/uploads/2009/06/michaelj.jpg
JE, ulikuwa na umri wa miaka mingapi wakati mfalme wa muziki wa Pop wa Marekani, hayati Michael Jackson alipoitembelea Tanzania mwaka 1992 na kufika shule maalum ya watoto yatima na wenye mtindio wa ubongo iliyopo Sinza?
Mwanamuziki huyo aliyekuwa maarufu zaidi duniani hadi anakufa 2009, alifika nchini akiwa balozi wa ziara ya Umoja wa Mataifa na akapokelewa kiserikali na Waziri wa Mambo ya Nje wakati huo, hayati Hassan Diria.
Michael Jackson alitua jioni moja uwanja wa ndege wa Dar akiwa amevalia shati la kijani lenye mikono mirefu, suruali nyeusi na kofia nyeusi, akapandishwa kwenye Mercedes iliyompeleka hadi Kilimanjaro Hotel (wakati huo) ambayo baadaye ikawa Kilimanjaro Hotel Kempinsk, sasa ikiitwa Hyatt Regency Dar es Salaam.
http://www.zenjydar.co.uk/2009months/200906/images/michael+jackson+diria.jpgMashabiki waliokuwa na habari walijazana uwanja wa ndege Dar  “kumkodolea mimacho” mwanamuziki huyo wakati huo akiwa na umri wa miaka 34 tu, mbali na wale waliomfuata hadi kwenye hoteli hiyo. Wakaungana na wale waliokuwa wakimsubiri hapo kumshangilia kwa mbinja na mayowe ya furaha.
Pia, mashabiki waliokuwa na habari za ujio na ratiba yake, walijitokeza kwa wingi na kumshangaa vilivyo, The Wacko Jacko alipotembelea shule hiyo ya Sinza, kesho yake.
Katika ziara yake hiyo ya siku mbili nchini, alikutana na mkuu wa nchi ambaye wakati huo alikuwa Rais Ali Hassan Mwinyi.
Ndivyo Michael Joseph Jackson alivyofika Tanzania na kushikana mikono na watoto wa Sinza miaka karibu 20 iliyopita!

BINTI MDOGO AGOMBEA MWANAUME

Binti ambaye umri wake unakadiriwa kuwa kati ya miaka 15-16, aliyefahamika kwa jina moja la Fatuma, amezua sekeseke la aina yake akidaiwa kugombea mwanaume.
Tukio hilo la aibu na kusikitisha lilitokea Februari 29, mwaka huu, saa nane mchana ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar.
Awali, Fatuma alionekana akiwa ameketi na mashosti zake wakipata ofa ya pombe kutoka kwa mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Peter ambapo baada ya muda alitokea demu mwingine na kwenda kukaa meza nyingine.
Ilidaiwa kuwa, yule msichana aliyetinga ukumbini pale alikuwa ni mpenzi wa Peter hivyo katika kuua soo, mwanaume huyo alimtuma mhudumu awapelekee fedha Fatuma na wenzake na kumtaka akawaambie wasimfuatefuate tena.
Baada ya Fatuma ambaye muda mwingi alikuwa akijua kuwa ndiye atakayeondoka na Peter kwa madai ni mzuri kuliko wenzake kuhisi anataka kuachwa solemba, alinyanyuka na kwenda kumletea ‘vagi’ yule demu aliyewatibulia.
Aidha, kibinti hicho kilimporomoshea matusi mazito Peter akimwambia eti anashobokea mademu wenye mititi makubwa wakati kigoli (yeye) yupo.
“Wewe nilikuona mjanja kumbe hauna lolote, mjinga na fala mkubwa wewe,” alisikika akibwatuka binti huyo.
Maneno hayo yaliamsha hasira kwa Peter ambaye alinyanyuka na kuanza kumshushia kipigo Fatuma kiasi cha kuzua timbwili zito na kujaza watu.
Hata hivyo, baadhi ya wasamaria wema waliokuwa eneo hilo waliingilia kati na kumuokoa binti huyo akiwa nyang’anyang’a kwa kipigo.
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi huo, binti huyo alisema: “Mimi namshangaa sana yule kaka, kunipiga bila sababu za msingi, kama ni ofa sijamuomba, amenipa mwenyewe, kwa nini anipige?” alihoji Fatuma huku akiondoka eneo hilo akiwa amenyong’onyea.
Mtumishi wa MUNGU mmoja akiwa kwenye gari alisimamishwa na Trafic Police,police
akiwa anahitaji rushwa alianza kuuliza maswali mengi, mara mbona
gari lako linatoa moshi mwingi? mbona gari lako matairi yameisha,
hatimaye polisi akamuamuru padre waende nae kituoni.
Njiani polisi alimuuliza , umesema wewe ni Mtumishi wa MUNGU, je unabiblia
ndani ya gari, akajibu ndio ninayo, polisi akamuambi...a ,
pack gari pembeni na unipe biblia. Mtumishi akapaki gari na kumpa biblia
yule polisi,Polisi akasita kupokea, akamwambia Mtumishi 'fungua na usome
Mathayo 5:25-26 "Mtu wa Mungu akasoma ":
"Patana na Mshtaki wako upesi,wakati uwapo pamoja naye njiani: yule mshtaki asijekukupeleka kwa kadhi na kadhi akakupeleka kwa askari,ukatupwa gerezani.
" Amin nakuambia,Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho"
Mtu wa Mungu akampa yaliyo yake kaizari.
Polisi akatabasamu na kusema 'msifanye migumu mioyo yenu".. Enenda kwa amani.

Thursday, March 1, 2012

http://api.ning.com/files/XDvieCk-6HgMCoWy-Xa5snZikZ4tAo3aaMjAvHl7RxRAPZ8eRira22pKg-WzdeZHspdHS18PcUYtO0eS4wtGM3CaNTC6EP*W/theopilkk.jpg

CHADEMA WAMCHAGUA NASSARI ARUMERU


 Joshua Nassari
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimemchagua Joshua Nassari kupeperusha bendera yake katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, utakaofanyika Aprili Mosi, mwaka huu.

Akitangaza matokeo ya uteuzi huo, Mkurugenzi wa Bunge na Oganaizesheni wa Chadema, John Mrema alisema Nassari ameteuliwa baada ya kupata kura 805 sawa na asilimia 90.6 ya kura zote 888 zilizopigwa.

Alisema Nassari aliwaangusha Anna Mghiwa aliyeshika nafasi ya pili kwa kupata kura 23, akifuatiwa na Godluv Simba (18), Rebecca Magwisha (12), Samweli Shami (10), Anthony Mussari (8) na Yohanne Kimuto (6).
“Kura zilizopigwa zilikuwa 888 zilizoharibika ni sita na wagombea wote wametangaza kukubali matokeo,” alisema Mrema. Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa ni mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei.
Ukumbini

Mgombea Musari aliyehamia Chadema baada ya kuangushwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea kupitia CCM aliwaambia wajumbe kwamba, tayari alikwishafukuzwa kazi ya ukuu wa shule hivyo aliomba wajumbe wampigie kura kupeperusha bendera ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini katika uchaguzi huo.

Kauli ya mgombea huyo ilimfanya mmoja wa wajumbe kutoka kata ya Maji ya Chai kumhoji iwapo hatahama tena Chadema akikosa kura katika uchaguzi huo wa jana, naye akaahidi kushirikiana na wana Chadema wenzake kutafuta ushindi wa chama chake hicho.

Awali, mzee Mtei alisema chama hicho kinahitaji wabunge wenye kuendesha na kutekeleza sera zinazojibu mahitaji ya
wananchi na jamii wanayoongoza kwa kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha wananchi wote bila kujali tofauti miongoni mwao.

“Hivi sasa wananchi wengi wanakula mlo mmoja kwa siku sababu hawawezi kumudu gharama ya milo miwili na hili linasababishwa na usimamizi na uongozi mbovu wa Serikali ya CCM,” alisema Mtei.

Aliwaasa wana Arumeru kupuuza rushwa inayodaiwa kuwa imeanza kusambazwa sehemu mbalimbali za jimbo hilo na wanaodaiwa kuwa viongozi au wanachama wa CCM na kuchagua kiongozi wanayeamini kuwa atawakilisha hoja na fikra zao bungeni bila kushaiwishiwa kwa rushwa.

CCM wakamatwa kwa rushwa
Katika hatua nyingine, viongozi watatu wa CCM, wanashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa kuhusiana na kura za maoni za marudio ndani ya chama hicho.
Kura za maoni zinatarajiwa kupigwa leo na wagombea wawili
walioongoza katika awamu ya kwanza ya kura za maoni zilizofanyika wiki iliyopita, Siyoi Sumari na Wililiam Sarakikya watapigiwa kura.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Arusha, Mbengwa Kasomambuto alithibitisha jana kwa simu kushikiliwa kwa viongozi hao ambao hata hivyo, alikataa kuwataja majina kwa sababu ya kiuchunguzi.

“Kweli tunawashikilia wana CCM watatu kwa mahojiano baada ya vijana wangu waliotapakaa kila sehemu ya Jimbo la Arumeru Mashariki kuwakuta katika mazingira yanayoashiria uwepo wa rushwa,” alisema...Soma zaidi www.mwananchi.co.tz