The DailyBest
news, breaking news, news blog, business, sports,story, politics, technology, entertainment, living
Monday, July 9, 2012
Wednesday, June 13, 2012
Wednesday, May 2, 2012
Wednesday, March 28, 2012
MCHUNGAJI ALIYEGEUKA MUUAJI-SEHEMU YA MWISHO
Muuaji John Nelson Canning
ILIPOISHIA..........
Ni
katika kipindi hicho ambapo ujenzi wakanisa hilo ulipoanza ndipo mauaji
ya Gleese na mkewe yalipotokea. Polisi wa upelelezi waliona ni vyema
wakaanza upelelezi wao kwa kuangalia vyanzo vyake vya mapato pamoja na
matumizi.
ENDELEA KUSOMA HAPA.................
Katika upelelezi wao ndipo walipokuja kugundua kwamba ndani ya wiki moja tangu mchungaji Canning apewe jukumu la kusimamia akaunt za familia ya Gleese ndipo alipolipa deni lake lote la manunuzi ya lile ghala aliloligeuza kuwa kanisa, na baada ya hapo akaanza matumizi makubwa ya fedha kwa kununua nyumba mbili zenye thamani ya dola 83,000, na wakati huo huo alianza upanuzi wa nyumba aliyokuwa akiishi kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi. Kwa muda mfupi akaunti za familia ya Gleese ilikuwa imekauka ikiwemo akaunti yao nyingine ya akiba iliyokuwa na kiasi cha dola 16,000, zilikuwa zimetoweka kusikojulikana.
Polisi wa upelelezi walipowahoji marafiki wa familia ya Gleese, walidai kwamba wiki moja kabla ya kuuwawa kwao mke wa Gleese bibi Hazel Gleese alianza kumtilia mashaka mchungaji Canning kuhusiana na namna anavyosimamia fedha zao. Bi Hazel aliwaambia majirani zake kwamba anapanga kwenda katika benki jijini New York walipoweka fedha zao ili kuonana na meneja wa benki ili kupata taarifa ya fedha zao kwa mwaka mzima, lakini ikiwa imebaki siku chache kabla ya bi Hazel kwenda benki wakakutwa waameuwawa na hiyo ilitokea baada ya familia hiyo kugundua kwamba mchungaji Canning alikuwa ameghushi sahihi zao na kujiandikia hundi ambapo alikuwa akijilipa yeye mwenyewe.
Polisi wa upelelezi waliamua kuhamishia upelelezi wao katika benki hiyo iliyoko katika jiji la New York ambapo walikwenda na zile taarifa za benki (Bank statements) walizozikuta zimesambaa sakafuni baada ya mauaji yale kutokea. Hata hivyo mapaka kufikia hapo, bado polisi walikuwa hawajpata ushahidi wa kina wa kumfungulia mchungaji Canning mashitaka kuhusiana na mauaji ya ajuza wale.
Msemaji
mwingine wa timu hiyo ya upelelezi wa Robert Glick alisema kwamba wanao
ushihidi mwingine kutoka kwa raia mwema anaeishi jirani na kanisa la
mchungaji Canning ambae alibainisha kwamba siku ile yalipotokea mauaji
alimuona mchungaji huyo akienda na kurudi mara kwa mara kwenye shimo la
taka lililoko jirani na kanisa hilo ambapo inasemekana kwamba huenda
alikuwa antafuta namna ya kuizika miili ya ajuza wale. Askari wa
upelelezi walipoenda kuchunguza nyumbani kwa mchungaji huyo walikuta saa
ya mkononi ambayo ilikuwa na matone ya damu, damu hiyo ilipochunguzwa
aktika maabara ilikuja kugundulika kuwa ilikuwa ni ya Leo Gleese. Mpaka
kufikia hapo Polisi wakawa na uhakika kwamba sasa wamembaini muuaji wa
Leo naENDELEA KUSOMA HAPA.................
Katika upelelezi wao ndipo walipokuja kugundua kwamba ndani ya wiki moja tangu mchungaji Canning apewe jukumu la kusimamia akaunt za familia ya Gleese ndipo alipolipa deni lake lote la manunuzi ya lile ghala aliloligeuza kuwa kanisa, na baada ya hapo akaanza matumizi makubwa ya fedha kwa kununua nyumba mbili zenye thamani ya dola 83,000, na wakati huo huo alianza upanuzi wa nyumba aliyokuwa akiishi kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi. Kwa muda mfupi akaunti za familia ya Gleese ilikuwa imekauka ikiwemo akaunti yao nyingine ya akiba iliyokuwa na kiasi cha dola 16,000, zilikuwa zimetoweka kusikojulikana.
Polisi wa upelelezi walipowahoji marafiki wa familia ya Gleese, walidai kwamba wiki moja kabla ya kuuwawa kwao mke wa Gleese bibi Hazel Gleese alianza kumtilia mashaka mchungaji Canning kuhusiana na namna anavyosimamia fedha zao. Bi Hazel aliwaambia majirani zake kwamba anapanga kwenda katika benki jijini New York walipoweka fedha zao ili kuonana na meneja wa benki ili kupata taarifa ya fedha zao kwa mwaka mzima, lakini ikiwa imebaki siku chache kabla ya bi Hazel kwenda benki wakakutwa waameuwawa na hiyo ilitokea baada ya familia hiyo kugundua kwamba mchungaji Canning alikuwa ameghushi sahihi zao na kujiandikia hundi ambapo alikuwa akijilipa yeye mwenyewe.
Polisi wa upelelezi waliamua kuhamishia upelelezi wao katika benki hiyo iliyoko katika jiji la New York ambapo walikwenda na zile taarifa za benki (Bank statements) walizozikuta zimesambaa sakafuni baada ya mauaji yale kutokea. Hata hivyo mapaka kufikia hapo, bado polisi walikuwa hawajpata ushahidi wa kina wa kumfungulia mchungaji Canning mashitaka kuhusiana na mauaji ya ajuza wale.
Hazel Gleese, nae si mwingine bali ni Mchungaji John Nelson Canning.
Siku chache baada ya kuongoza mazishi ya ajuza wale mchungaji Canning alikamatwa na kushitakiwa kwa mauaji ya ajuza wale. Katika kesi hiyo mchungaji Canning alikiri kuwa aliwauwa Leo na mkewe Hazel Gleese kwa kuwapiga kwa kitu kizito na kisha kuwanyonga usiku wa Januari 3, 1995, hiyo ilitokea baada ya kuwa amebanwa na ajuza hao kuhusiana na namna alivyotumia fedha zao huku wakimuonyesha taarifa ya benki inayoonyesha kwamba alijiandikia hundi na kujilipa yeye mwenyewe.
Mnamo Februari 1996 mchungaji John Nelson Canning alipatikana na hatia ya kuhusika na mauaji ya Leo na Hazel Gleese ambapo alihukumiwa kifungo cha maisha jela bila ya uwezekano wa kupata msamaha wa kifungo cha nje (Parole). Mara baada ya kusomwa hukumu hiyo msemaji wa Polisi Phil Ramer aliwaambia wandishi wa habari kwamba hili ni tukio ambalo hatakuja kulisahau katika maisha yake.
Kwa maneno yake mwenyewe alisema “ni vyema watu wakawa waaminifu, ni jambo la kushangaza kukuta mchungaji ambae ameaminiwa na waumini wake kisha anakuja kuwaua baadae kwa sababu ya pesa”
*********************MWISHO*******************
Tuesday, March 27, 2012
MCHUNGAJI ALIYEGEUKA MUUAJI
Muuaji John Nelson Canning
Mnamo January 3, 1995 mchungaji mmoja aitwae John Nelson Canning alikwenda katika kituo cha Polisi cha mji mdogo wa Sebring ulioko katika jimbo la Florida nchini Marekani na kutoa taarifa juu ya mauaji ya vikongwe wawili mtu na mkewe Bwana Leo na bibi Hazel Gleese.
Mchungaji huyo aliyekuwa na umri wa miaka 59 wakati huo aliwaeleza Polisi kwamba aligundua mauaji hayo baada ya kuwa amewatembelea nyumbani kwao kama ilivyo kawaida yake ya kuwatembelea waumini wake na kukuta miili ya vikongwe hao ikiwa imelala sakafuni kwenye dimbwi la damu.
Mchungaji Canning aliendelea kuwaeleza Polisi kwamba bwana na bibi Gleese ni waumini wa siku nyingi katika kanisa la Fountain of life ambalo yeye ni muanzilishi wake. Mchungaji huyo alibainisha kwamba katika kipindi cha miaka ya karibuni alikuwa ni muangalizi wa vikongwe hao ambao hawakubahatika kupata watoto katika maisha yao ya ndoa ambapo waliamua kumuasili mchungaji huyo na kumfanya mtoto wao na hivyo akawa anawaita Baba na Mama. Mara baada ya kupata taarifa hizo Polisi walikimbilia kwenye eneo la tukio na kukutana na hali ya kutisha katika eneo la tukio ambayo hawatakuja kuisahau.
Kwani waliukuta mwili wa Bibi Hazel Gleese ambae alikuwa na umri wa miaka 90 wakati huo umelala jikoni ukiwa umetapakaa damu. Na mwili wa mumewe leo Gleese nao pia ulikutwa ukiwa umeegemea ukuta wa chumbani. Wote walikuwa wanaonyesha kwamba walikuwa wamepigwa na kunyongwa. Katika eneo ambalo miili ya ajuza wale ililala polisi wa upelelezi walikuta pia baadhi ya nyaraka za kibenki zikiwa zimesambaa pale sakafuni huku baadhi ya nyaraka hizo zikiwa zimelowana kwa damu, pia kulikuwa na dalili zote kwamba bibi kulikuwa na purukushani za kupigana kati ya bibi Gleese na mtuhumiwa au watuhumiwa wa mauaji. Siku ya mazishi ya maajuza hao umati mkubwa wa watu wa mji wa Sebring walihudhuria mazishi hayo yaliyoongozwa na mchungaji John Nelson Canning.
Familia ya Gleese haikubahatika kupata watoto katika maisha yao ya ndoa ndio sababu waliamua kuwaasili Canning na mkewe Judy hapo mnamo mwaka 1994. Hata hivyo wakati wa mazishi hayo bado Polisi wa upelelezi walianza kumtilia mashaka mchungaji huyo kwa kumhusisha na mauaji ya ajuza wale.
Polisi hao wa upelelezi walianza kumtilia mashaka mchungaji Canning tangu siku ile ya kwanza alipokwenda kutoa taarifa ya kutokea kwa mauaji ya ajuza wale ambao aliwachukulia kama wazazi wake. Akiandikisha maelezo yake Polisi namna alivyogundua mauaji ya Bi hazel na bwana Leo Gleese, Canning aliwaeleza Polisi akiwa katika hali ya kawaida kabisa. Kwa maneno yake mwenyewe Canning alisema “kwa kweli niligundua mauaji hayo jana asubuhi”
Polisi wa upelelezi walistushwa na habari hizo, kwani kwa mujibu wa maelezo yake ilionyesha kuwa miili ya Hazel na Leo Gleese ilikuwa imelala pale sakafuni kwa masaa 24 tangu kuuwawa pamoja na kuwa mchungaji Canning alifahamu kuhusu kutokea mauaji tangu jana asubuhi. Alipoulizwa kwamba kwa nini hakutoa taarifa mapema, mchungaji Canning alidai kwamba aliogopa kutoa taarifa kwa sababu hapakuwa na shahidi mwingine zaidi yake, hivyo aliogopa kuwa mtuhumiwa wa kwanza kuhusishwa na mauaji yale.
Kwa maneno yake mwenyewe Canning alsema “ Niliingia ndani na kustushwa na mauaji yale, nilichanganyikiwa na kufunga mlango kisha nikaondoka kwani niliogopa kutoa taarifa za vifo hivi kwa kuhofia kwamba nitahusishwa navyo mpaka leo ndio nikakata shauri nije nitoe taarifa” Mchungaji Cunning aliendelea kuwaambia polisi wa upelelezi kwamba akiwa ameshikwa na kihoro alishinda kutwa nzima akifikiria jinsi atavyotoa taarifa za vifo vile. Alipoulizwa kwamba siku hiyo ya kihoro aliitumia akiwa wapi, Mchungaji Canning aliwashangaza polisi kwa kuwaambia kuwa alishinda ufukweni mwa Bahari akiwa na marafiki zake na kisha usiku wakaungana pamoja kwenye mghahawa mmoja kwa ajili ya kupata mlo wa usiku.
Kwa ujumla maelezo ya Mchungaji Canning yalikuwa yanatia mashaka kwani Polisi wa upelelezi walibaki wakijiuliza kuwa, hivi hiyo ndio tabia ya mtu aliyeshuhudia mauaji ya kikatili ya watu ambao aliwafanya kuwa wazazi wake? Kuanzia hapo Polisi wa upelelezi walianza kumuhoji Mchungaji Canning kwa makini zaidi. Msemaji wa Polisi Phil Ramer akizungumza na waandishi wa habari alisema “Kama inamchukuwa mtu siku nzima kutoa taarifa za vifo vya watu wanaomuhusu waliouwawa kikatili, hiyo haiwezi kuwachukuwa wanasayansi wa kutengeneza Roketi kugundua kwamba muuaji nai nani”
Kwani kwa jinsi Canning anavyojieleza, ndivyo anavyozidi kudhihirisha kwamba kuna jambo analificha kuhusiana na mauaji hayo, alibainisha askari wa upelelezi anaeongoza timu ya wapelelezi wanaochunguza mauaji hayo Sajent Steven Carr. Kwa muda mfupi wapelelezi wa polisi walikuja kugungua kuwa Mchungaji Canning na Familia ya Gleese walikuwa na uhusiano wa karibu sana.
Historia inaonyesha kuwa awali Mchungaji Canning alikuwa ni ni Mchungaji wa kanisa moja lilipo katika mji wa Maine lakini baadae akaja akahamia katika mji wa Sebring na kuanzisha kanisa lake mwenyewe aliloliita Fountain of life hapo mnamo mwaka 1980. Miongoni mwa waumini wa kanisa hilo kulikuwa na wazee zaidi ya 50 ambao walikuwa ni wafuatiliaji wazuri wa mahubiri ya mchungaji Canning kupitia luninga kabla ya kujiunga na kanisa hilo.
Hapo ndipo kwa mara ya kwanza ilipotokea Leo Gleese mhasibu mstaafu na mkewe Hazel mwana mitindo wa zamani kujuana na mchungaji Canning.
Ni katika kipindi hicho ndipo familia ya Gleese ilipomuasili mchungaji Canning na mkewe na kuwaamini kiasi cha kuwafanya kama watoto wao ambapo kutokana na hali zao kuwa dhaifu kwa sababu ya uzee walimpa mamlaka ya kumiliki akaunti zao na kuwa mshauri wa familia hiyo katika maswala ya kifedha, kosa ambalo lilikuja kuwagharmu maisha yao. Pia polisi wa upelelezi walikuja kugundua kwamba mchungaji Canning hakuwa ameaminiwa na familia ya Gleese tu bali pia waumini wengi katika kanisa lake walimuamini na kumfanya mshauri wao wa maswala ya kifedha.
Pia wapelelezi hao wa polisi walikuja kushangaa baada ya kugundua kuwa kw takribani miaka 15 kanisa la Fountain of life lilikuwa likiendeshwa katika ghala chakavu alilolinunua mara baada ya kuhamia Sebring, na katika kipindi cha miaka kadhaa mchungaji Canning alikuwa akichangisha fedha kwa waumini wake ili ajenge jingo la kisasa la kanisa lake ambalo mwenyewe alisema litakuwa ni la karne. Ni katika kipindi hicho ambapo ujenzi wakanisa hilo ulipoanza ndipo mauaji ya Gleese na mkewe yalipotokea. Polisi wa upelelezi waliona ni vyema wakaanza upelelezi wao kwa kuangalia vyanzo vyake vya mapato pamoja na matumizi.
Mnamo January 3, 1995 mchungaji mmoja aitwae John Nelson Canning alikwenda katika kituo cha Polisi cha mji mdogo wa Sebring ulioko katika jimbo la Florida nchini Marekani na kutoa taarifa juu ya mauaji ya vikongwe wawili mtu na mkewe Bwana Leo na bibi Hazel Gleese.
Mchungaji huyo aliyekuwa na umri wa miaka 59 wakati huo aliwaeleza Polisi kwamba aligundua mauaji hayo baada ya kuwa amewatembelea nyumbani kwao kama ilivyo kawaida yake ya kuwatembelea waumini wake na kukuta miili ya vikongwe hao ikiwa imelala sakafuni kwenye dimbwi la damu.
Mchungaji Canning aliendelea kuwaeleza Polisi kwamba bwana na bibi Gleese ni waumini wa siku nyingi katika kanisa la Fountain of life ambalo yeye ni muanzilishi wake. Mchungaji huyo alibainisha kwamba katika kipindi cha miaka ya karibuni alikuwa ni muangalizi wa vikongwe hao ambao hawakubahatika kupata watoto katika maisha yao ya ndoa ambapo waliamua kumuasili mchungaji huyo na kumfanya mtoto wao na hivyo akawa anawaita Baba na Mama. Mara baada ya kupata taarifa hizo Polisi walikimbilia kwenye eneo la tukio na kukutana na hali ya kutisha katika eneo la tukio ambayo hawatakuja kuisahau.
Kwani waliukuta mwili wa Bibi Hazel Gleese ambae alikuwa na umri wa miaka 90 wakati huo umelala jikoni ukiwa umetapakaa damu. Na mwili wa mumewe leo Gleese nao pia ulikutwa ukiwa umeegemea ukuta wa chumbani. Wote walikuwa wanaonyesha kwamba walikuwa wamepigwa na kunyongwa. Katika eneo ambalo miili ya ajuza wale ililala polisi wa upelelezi walikuta pia baadhi ya nyaraka za kibenki zikiwa zimesambaa pale sakafuni huku baadhi ya nyaraka hizo zikiwa zimelowana kwa damu, pia kulikuwa na dalili zote kwamba bibi kulikuwa na purukushani za kupigana kati ya bibi Gleese na mtuhumiwa au watuhumiwa wa mauaji. Siku ya mazishi ya maajuza hao umati mkubwa wa watu wa mji wa Sebring walihudhuria mazishi hayo yaliyoongozwa na mchungaji John Nelson Canning.
Akiongoza
mazishi hayo mchungaji Canning, kwa maneno yake mwenyewe alisema
“Miongoni mwenu mlikuwa marafiki wa muda mrefu wa baba na mama yangu
hawa, lakini ninayo mashaka kwamba yupo mtu yeyote aliyekuwa karibu na
na familia hii zaidi yangu na mke wangu”
Huku akitokwa na machozi, mchungaji huyo aliendelea kusema “Najivunia familia ya ajuza hawa kuniomba waniasili (Adopt) niwe mtoto wao, na nilijivunia kuwaita baba na mama kama wazazi wangu”
Huku akitokwa na machozi, mchungaji huyo aliendelea kusema “Najivunia familia ya ajuza hawa kuniomba waniasili (Adopt) niwe mtoto wao, na nilijivunia kuwaita baba na mama kama wazazi wangu”
Familia ya Gleese haikubahatika kupata watoto katika maisha yao ya ndoa ndio sababu waliamua kuwaasili Canning na mkewe Judy hapo mnamo mwaka 1994. Hata hivyo wakati wa mazishi hayo bado Polisi wa upelelezi walianza kumtilia mashaka mchungaji huyo kwa kumhusisha na mauaji ya ajuza wale.
Polisi hao wa upelelezi walianza kumtilia mashaka mchungaji Canning tangu siku ile ya kwanza alipokwenda kutoa taarifa ya kutokea kwa mauaji ya ajuza wale ambao aliwachukulia kama wazazi wake. Akiandikisha maelezo yake Polisi namna alivyogundua mauaji ya Bi hazel na bwana Leo Gleese, Canning aliwaeleza Polisi akiwa katika hali ya kawaida kabisa. Kwa maneno yake mwenyewe Canning alisema “kwa kweli niligundua mauaji hayo jana asubuhi”
Polisi wa upelelezi walistushwa na habari hizo, kwani kwa mujibu wa maelezo yake ilionyesha kuwa miili ya Hazel na Leo Gleese ilikuwa imelala pale sakafuni kwa masaa 24 tangu kuuwawa pamoja na kuwa mchungaji Canning alifahamu kuhusu kutokea mauaji tangu jana asubuhi. Alipoulizwa kwamba kwa nini hakutoa taarifa mapema, mchungaji Canning alidai kwamba aliogopa kutoa taarifa kwa sababu hapakuwa na shahidi mwingine zaidi yake, hivyo aliogopa kuwa mtuhumiwa wa kwanza kuhusishwa na mauaji yale.
Kwa maneno yake mwenyewe Canning alsema “ Niliingia ndani na kustushwa na mauaji yale, nilichanganyikiwa na kufunga mlango kisha nikaondoka kwani niliogopa kutoa taarifa za vifo hivi kwa kuhofia kwamba nitahusishwa navyo mpaka leo ndio nikakata shauri nije nitoe taarifa” Mchungaji Cunning aliendelea kuwaambia polisi wa upelelezi kwamba akiwa ameshikwa na kihoro alishinda kutwa nzima akifikiria jinsi atavyotoa taarifa za vifo vile. Alipoulizwa kwamba siku hiyo ya kihoro aliitumia akiwa wapi, Mchungaji Canning aliwashangaza polisi kwa kuwaambia kuwa alishinda ufukweni mwa Bahari akiwa na marafiki zake na kisha usiku wakaungana pamoja kwenye mghahawa mmoja kwa ajili ya kupata mlo wa usiku.
Kwa ujumla maelezo ya Mchungaji Canning yalikuwa yanatia mashaka kwani Polisi wa upelelezi walibaki wakijiuliza kuwa, hivi hiyo ndio tabia ya mtu aliyeshuhudia mauaji ya kikatili ya watu ambao aliwafanya kuwa wazazi wake? Kuanzia hapo Polisi wa upelelezi walianza kumuhoji Mchungaji Canning kwa makini zaidi. Msemaji wa Polisi Phil Ramer akizungumza na waandishi wa habari alisema “Kama inamchukuwa mtu siku nzima kutoa taarifa za vifo vya watu wanaomuhusu waliouwawa kikatili, hiyo haiwezi kuwachukuwa wanasayansi wa kutengeneza Roketi kugundua kwamba muuaji nai nani”
Kwani kwa jinsi Canning anavyojieleza, ndivyo anavyozidi kudhihirisha kwamba kuna jambo analificha kuhusiana na mauaji hayo, alibainisha askari wa upelelezi anaeongoza timu ya wapelelezi wanaochunguza mauaji hayo Sajent Steven Carr. Kwa muda mfupi wapelelezi wa polisi walikuja kugungua kuwa Mchungaji Canning na Familia ya Gleese walikuwa na uhusiano wa karibu sana.
Historia inaonyesha kuwa awali Mchungaji Canning alikuwa ni ni Mchungaji wa kanisa moja lilipo katika mji wa Maine lakini baadae akaja akahamia katika mji wa Sebring na kuanzisha kanisa lake mwenyewe aliloliita Fountain of life hapo mnamo mwaka 1980. Miongoni mwa waumini wa kanisa hilo kulikuwa na wazee zaidi ya 50 ambao walikuwa ni wafuatiliaji wazuri wa mahubiri ya mchungaji Canning kupitia luninga kabla ya kujiunga na kanisa hilo.
Hapo ndipo kwa mara ya kwanza ilipotokea Leo Gleese mhasibu mstaafu na mkewe Hazel mwana mitindo wa zamani kujuana na mchungaji Canning.
Ni katika kipindi hicho ndipo familia ya Gleese ilipomuasili mchungaji Canning na mkewe na kuwaamini kiasi cha kuwafanya kama watoto wao ambapo kutokana na hali zao kuwa dhaifu kwa sababu ya uzee walimpa mamlaka ya kumiliki akaunti zao na kuwa mshauri wa familia hiyo katika maswala ya kifedha, kosa ambalo lilikuja kuwagharmu maisha yao. Pia polisi wa upelelezi walikuja kugundua kwamba mchungaji Canning hakuwa ameaminiwa na familia ya Gleese tu bali pia waumini wengi katika kanisa lake walimuamini na kumfanya mshauri wao wa maswala ya kifedha.
Pia wapelelezi hao wa polisi walikuja kushangaa baada ya kugundua kuwa kw takribani miaka 15 kanisa la Fountain of life lilikuwa likiendeshwa katika ghala chakavu alilolinunua mara baada ya kuhamia Sebring, na katika kipindi cha miaka kadhaa mchungaji Canning alikuwa akichangisha fedha kwa waumini wake ili ajenge jingo la kisasa la kanisa lake ambalo mwenyewe alisema litakuwa ni la karne. Ni katika kipindi hicho ambapo ujenzi wakanisa hilo ulipoanza ndipo mauaji ya Gleese na mkewe yalipotokea. Polisi wa upelelezi waliona ni vyema wakaanza upelelezi wao kwa kuangalia vyanzo vyake vya mapato pamoja na matumizi.
ITAENDELEA KESHO................
Friday, March 23, 2012
ASPIRINI INAWEZA KUZUIA SARATANI
Vidonge vya Asprin |
Kumeza kidonge cha aspirini kila siku inaweza kuzuia na hata kutibu saratani. Taraifa hii ni kwa mujibu wa utafiti mpya.
Matokeo
ya utafiti huo yalichapishwa na jarida la matibabu la The Lancet, na
hivyo kuzidisha kuonyesha manufaa ya aspirini katika matibabu ya
saratani.
Watu wengi tayari wanatumia Aspirini kama dawa ya maradhi ya moyo.
Lakini
wataalamu wanaonya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuelezea watu
kutumia aspirin ili kuzuia saratani na hata vifo vinavyotokana na
saratani.
Wataalamu hao wanaonya kuwa dawa hiyo inaweza kusababisha athari kubwa kama kuvuja damu tumboni.
Prof
Peter Rothwell,wa chuo kikuu cha Oxford akiwa na wakufunzi wengine
ambao wamefanya utafiti wa hivi karibuni, tayari walikuwa wamehusisha
aspirin na kuzuia aina ya saratani hasa saratani ya matumbo.
Lakini
utafiti wao wa awali, ulipendekeza kuwa watu wanahitaji kutumia dawa
hiyo kwa takriban miaka 10 ili iweze kufanya kazi hiyo.
Sasa
wataalamu wanaamini kuwa uwezo wa dawa hiyo kuzuia saratani, hutokea
mapema mno kati ya miaka mitatu na mitano. Hii ni kwa mujibu wa taarifa
mpya kutoka kwa majaribio 51 yaliyohusisha wagonjwa 77,000.
Na
asprini haionekani tu kuzuia tisho la kuugua aina nyingi ya saratani
bali pia lakini pia inazuia saratani kusambaa kwa sehemu zingine
mwilini.
Hata hivyo majaribio hayo hayakufananisha dawa ya aspirini na dawa zengine zinazoweza kuzuia maradhi ya moyo.
Lakini
wakati kikundi cha wataalamu, kilichoongozwa na Profesa Rothwel
kilidurusu wangapi kati ya watu waliohusika katika utafiti huo walipata
kuugua saratani na hata kufariki kutokana na ugonjwa huo, waligundua
kuwa vifo vilitokana pia na matumizi ya aspirin.
Kuzuia kusambaa kwa Saratani
Kwa
mtu anayetumia kiwango kidogo cha dawa hiyo kila siku, ilionekana
kupunguza idadi ya visa vya saratani kwa robo baada ya miaka mitatu
pekee.
Ni
watu tisa waliogungulika kuwa na saratani katika watu elfu moja kila
mwaka ikilinganishwa na watu kumi na mbili kwa watu elfu moja kwa wale
waliomeza tembe hizo.
Pia ilipunguza idadi ya vifo vilivyookana na saratani kwa asilimia kumi na tano.
source:BBC
Thursday, March 8, 2012
MGOMO WA MADAKTARI WAANZA TENA
Baadhi
ya wagonjwa waliopo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili wakisubiri
huduma katika Kitengo cha Mifupa (MOI), huku wakiwa hawajui hatma yao
baada ya madaktari kuanza mgomo wao kwa mara nyingine tena leo.
ULE
mgomo wa madaktari uliotangazwa kufanyika leo umeanza katika mazingira
ya kimyakimya. Hii imebainika pale mpekuzi wetu alipotembelea hospitali
hiyo ili kujionea kile kichokuwa kimekusudiwa.
Hali
ilivyokuwa katika hospitali hiyo kuu ya taifa kwa siku ya leo ni
kwamba hakuna daktari hata mmoja aliyekuwa anashughulika na mgonjwa bali
manesi tu ndiyo waliokuwa wanashughulika na wagonjwa wa zamani na si
wapya ambapo.
Uchunguzi
uliofanywa hospitalini hapo ni kuwa kila idara ilikuwa na mikutano
katika kujadili hotuba ya waziri mkuu aliyoitoa jana ikiwa inalenga
kuwasihi madaktari waache mgomo bali waendelee kufanya kazi huku suala
lao likiwa linashughulikiwa.
Kwa
upande wa madakari hao wameazimia kwa pamoja kuwa mgomo huo unaanza
rasmi leo baada ya kikao hicho na kuwataka wananchi wawaelewe kuwa
lengo lao ni kuboresha maslahi yao.
Kwa
mara nyingine Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema kama wanakusudia
kufanya mgomo huo basi serikali imejiandaa kwa kila hali ili
kukabiliana na mgomo huo.
Katika
mazingira ambayo yanaweza kuitwa tata siku ya kesho haileweki hali
itakuwaje kitu ambacho wagonjwa wengi wamepewa tarehe za mbele hali
ambayo wengi wao imesononeshwa na ahadi hizo.
Mpekuzi
wetu alipojaribu kumtafuta msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,
Ameniel Aligalesha, aliambiwa kuwa yupo katika kikao ndani ya hospitali
hiyo na lengo lilikuwa ni kujadili na kufikia maamuzi ya hotuba ya
waziri mkuu.
Hadi
leo Pinda ameishakaa mikutano mbalimbali kujadili swala hilo la
madaktari. Kwa mara ya kwanza ilikuwa Januari 29 mwaka huu katika
ukumbi wa Karemjee aliposema kuwa daktari ambaye angegome
angejifukuzisha kazi na akapiga marufuku mikutano yao kufanyika kokote.
Februari 9 alikutana na madakari bingwa na watumishi wa hospitali za Temeke, Ilala, Mwananyamala na Muhimbili.
Na
jana alikutana na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo aliyakataa
masharti ya madaktari ambayo waliyatoa ili waweze kuendelea na
mazungumzo na serikali.
Baada ya madaktari kukaa leo, Pinda amesema kama wametangaza mgomo serikali iko tayari kukabiliana na mgomo huo.
Subscribe to:
Posts (Atom)