KANISA
moja huko Mlandizi, wilayani Bagamoyo, Pwani, limeingia katika kashfa
ya kuwatapeli mamilioni ya fedha waumini wake kwa kisingizio cha
kuziombea fedha ili kuondoa mikosi kwa kuzifanyia ibada ya utakaso.
Uchunguzi wa gazeti hili umeonyesha kuwa ibada katika kanisa hilo,
inafanyika ili kuwaombea watu wenye matatizo ya fedha na magonjwa.
Kwa
mujibu wa uchunguzi huo, fedha zinazoletwa kwa ajili ya kuombewa,
zinawekwa kwenye sanduku maalumu linaojulikana kuwa ni sanduku la agano
na baadaye kuombewa kwa muda kabla kuzirejesha kwa muumini.
Mmoja
wa waumini waliodai kuibiwa fedha zao, kwa njia hiyo na ambaye
hakutaka jina ake litajwe gazetini, alidai kuwa analidai kanisa Sh20
milioni, alizozitoa kwa nyakati tofauti ili ziombewe.
“Nilimpa
mtumishi fedha ili aziombee na kuzifanyia utakaso kwa sababu alisema
mara nyingi fedha tunazotumia zina mashetani,” alisema muumini huyo
ambaye ni mwanamke.
“Unajua
kuna wakati mtu unafanya biashara lakini, haitoki, hupati faida, sasa
watumishi wa Mungu wanasema kunakuwa na mikosi kama vile chuma ulete.
Ndiyo maana nilimkabidhi aziombee,” alisema.
“Mara
ya kwanza nilipojiunga nilitoa Sh 600,000 ambazo aliziombea na baada ya
miezi minne alinirudishia. Mara ya pili nilikuwa nasafirisha mzigo wa
thamani ya Sh 7.5 milioni kwenda Zimbabwe. Siku hiyo walikuja dukani
kwangu Kariakoo na kuniambia kuwa itabidi nitoe fungu la kumi la mzigo
huo yaani Sh750,000 ambazo hata hivyo, walisema watanirudishia,”
alisema.
“Kwa
kuwa sikuwa na fedha hizo nililazimika kukopa nikijua kuwa
watazirudisha kabla sijasafiri. Kesho yake nilipozifuatilia Mlandizi
nikakuta wamesafiri kwenda Moshi, ila wameniachia Sh 75,000 wakisema
hilo ndiyo fungu la 10 langu.”
Alisema
kiongozi huyo wa kanisa na wenzake walimpa masharti ya kutoa ‘chenji’
fedha atakazopata faida isipokuwa nauli, pesa ya kulipa hoteli na ya
chakula tu. Alidai kuwa alipotoka Zimbabwe, watumishi hao walimpigia
simu wakimtaka akutane nao Makambako, mkoani Iringa kwa madai kuwa Roho
Mtakatibu amewaagiza wakafanyie ibada katika mji huo.
Alisema
ingawa ya hakuwa na fedha za Kitanzania lakini kwa faida ya Dola 4,800
alizopata kwenye biashara zake, aliwatii na kushukia Makambako.
“Pale
Makambako ndiyo nyumbani kwa wazazi wa huyo mtumishi, tulifanya ibada
kuanzia saa saba usiku. Wakaniambia nitoe fedha zote nilizonazo ili
waziombee. Nikamwambia itabidi azirudishe mapema kwa sababu nilikuwa na
order ya kupeleka mzigo nchini Zambia. Akasema atazirudisha mapema,”
alidai muumini huyo.
Alidai
kuwa walikaa Iringa kwa muda wa siku tatu na kwamba waliporudi Dar es
Salaam, mtumishi alianza kumzungusha licha ya kukumbushwa kila mara.
“Badala ya kurudisha fedha kama tulivyokubaliana, alinipigia simu
akisema twende kwenye maombi Mlandizi saa saba usiku. Huko tena akasema
zile fedha itabidi ziombewe kwa siku saba zaidi. Siku saba zilipokwisha
bado alisema ameambiwa na Roho Mtakatibu kuwa fedha zikae kwenye Sanduku
la Agano kwa siku 21 zaidi,” alidai.
Alidai kuwa wakati wakiendelea kusubiri siku hizo, mtumishi alimshauri asiendelee tena kufanya biashara.
Kwa
mujibu wa mtu huyo, pamoja na kuzungushwa lakini bado aliendelea
kumwamini mtumishi kiasi cha kumpa fedha nyingine alizotaka.
Alisema
kijana mmoja wa Kitanzania anayeishi naye alitaka kufanyiwa maombi ili
mambo yake ya mwendee vizuri na kwamba yeye alimshawishi aje kufanyiwa
maombi kwenye kanisa hilo.
“Yule
kijana akaja kutoka Zimbabwe kwa ajili ya maombi hayo Siku hiyo
mtumishi alikuja nyumbani Kinondoni. nikamtambulisha mgeni wangu kwake.
Baada ya kusalimiana, alimwita kisha akamuuliza, una fedha hapo mfukoni.
kijana akasita kwanza halafu akaja nje kuniuliza, ‘huyo mama anauliza
kama nina fedha mfukoni lakini nimeshindwa kumjibu’. Mimi nikamwambia
ampe tu” alisema.
Kwa
mujibu wa muumini huyo, kijana huyo alikuwa na a Dola 5,900 na Randi
1,000 ambazo zote aliamriwa kumkabidhi mtumishi kwa maelezo kwamba
zinakwenda kuombewa na baadaye kurejeshwa.
Taratibu
za ibada Habari zimeeleza kuwa ibada katika kanisa hilo inategemea
uongozi wa Roho Mtakatifu na hakuna ratiba maalumu.
Mmoja wa wawatumishi wa kanisa hilo (jina tunalo), alisema hakuna ratiba maalumu hadi pale roho wa bwana atakavyowaambia.
“Hii
ni huduma ya maombezi ambayo ukija hapa, tunakuuliza mahitaji yako,
kisha tunakufanyia maombi. Unajua sisi hatuombi kama makanisa mengine.
Tunafuatilia mzizi wa tatizo la mtu tangu kizazi cha kwanza. Kama wewe
hukufanya matambiko na maagano, inawezekana wazazi wako au hata babu
zako. Hayo yote tunayavunja kwa jina la Yesu. Muda wa maombi utategemea
uzito wa tatizo,” alisema Kuhani huyo.
Baadhi
ya watu walioko karibu na kanisa hilo, walisema misururu ya magari
imekuwa ikufurika ikiwa na watu wanaofanya ibada katika kanisa hilo hasa
nyakati za usiku.
“Hapa
kila siku wanakuja matajiri na magari yao ili kuombewa na mara nyingi
ibada zinafanyika usiku,” alisema mwana kijiji ambaye hakutaka jina lake
liandikwe gazetini. Siku ya maombi Akisimulia jinsi ibada ya
kumwombea kijana huyo ilivyofanyika, mwanamke huyo alisema waliandaa
mbuzi, maziwa, pombe ya mbege, mvinyo, vitambaa vya rangi mbalimbali,
mtama na ulezi.
“Alisema
vitu vyote hivyo ni kwa ajili ya kutengua laana alizowekewa na mababu
zake. Ibada ilifanyika usiku wa manane huku yule kijana akiogeshwa kwa
mvinyo, uliochanganywa na damu ya mbuzi na sarafu za amani huku
akiombewa. Baadaye vile vitu vilichanganywa na biblia mpya na kufukiwa
kwenye shimo. Yule kijana alioga na kwenda kupumzika. Hata hivyo, ibada
iliendelea kwa siku tatu.” Alisema baadaye kijana aliambiwa asubiri
kwa muda wa siku 21 ndipo akachukue fedha zake huku akitakiwa kujitakasa
ndani ya siku hizo, lakini hadi sasa hajapata fedah hizo.
Sanduku
la agano Kwa mujibu wa mwanamke huyo, baada ya kutoa taarifa katika
Kituo cha Polisi Oysterbay na Polisi Mlandizi, alipewa ushirikiano
iliowezesha kumkamata huyo mtumishi huku wakifuatilia kilichomo ndani ya
Sanduku la Agano. “Siku hiyo tulikwenda na polisi kwenye kanisa hilo
usiku, wakalitafuta bila mafanikio. Ikabidi waondoke. Ila wakati
tunaondoka nilitumiwa ujumbe mfupi na mmoja wa waumini kuwa limefukiwa
karibu na madhabahu.
Alisema
siku iliyofuata polisi walilifukua na kulipata na kwamba walipolifungua
walikuta bahasha nyingi, msalaba, Biblia, kitabu cha Tenzi za rohoni na
fimbo.
Muumini
mwingine wa kiume, ambaye pia ni mfanyabiashara naye alidai kutapeliwa
Sh1.2 milioni alizoambiwa kuwa ni kwa ajili ya ‘Baraka za Ibrahim’ yaani
makabila 12 ya Israel.............