Saturday, February 11, 2012

ALICHOSEMA DIAMOND KUHUSU WALIOJITOA TUZO ZA KILI!


Profesa Jay, Diamond, mwana FA na AY wakati wakimpongeza Diamond aliposhinda tuzo tatu za KTMA 2010.
Baada ya mwimbaji Dully Sykes pamoja na rapa Jaffarai kutangaza msimamo wao wa kujitoa au kutotaka kushirikishwa kwenye tuzo za KTMA, Staa wa muziki Tanzania ambae anatajwa kuongoza kwenye mauzo ya showz, album na mengine, Diamond Platnums ametoa maoni yake kuhusu uamuzi wa wasanii wenzake.
Amesema “tatizo ni kwamba kila mwanamuziki ana njia yake anaitafutia hela mpaka muziki wake unajulikana mpaka anafika alipo, huwezi kujua kapitia wapi ndio maana kwa kila uamuzi atakao utoa inabidi niuheshimu japo wakati mwingine naona kama wanakosea lakini pia hawakosei, yani A na B yote majibu”
Diamond amesema hawezi kuwashauri chochote kwa sababu hao wasanii ni wakubwa zake kimuziki, kawakuta na siwezi nikawa mtu wa kuwashauri wao japo mdogo anaweza kumshauri mkubwa”
kuhusu wasanii walioshirikishwa kwenye TUZO za mwaka huu Diamond amesema anaona ni halali kwa sababu waliowachagua wanaufahamu muziki na mapungufu yoyote yaliyojitokeza wakubaliane nayo tu kwa sababu hakuna kisichokua na kasoro.

No comments:

Post a Comment