Inavyoanza
kuonekana kwa sasa vyama hivi pekee ndivyo vitakuwa vikimenyana kwenye
chaguzi kubwa.ni kama marekani.Naambiwa kule japo kuna vyama vingi sana
vidogo hata vya kikomunisti,lakini nyote mnajua kuwa kwa karne sasa ni
Republicans na Democrats pekee wanaotawala hasa siasa za nchi
hiyo.Mwenendo ulivyo kwa sasa hapa nchini Ni CHADEMA na CCM. Tangu
uchaguzi wa 2005 dalili hizi zilianza kuonekana hasa bungeni ambapo
ungedhani kulikuwa na wabunge wa vyama hivyo pekee.japo CUF kiliongoza
upinzani bungeni lakini kwa maoni yangu ni wabunge wa CHADEMA wale 11
waliojenga taswira ya upinzani.uchaguzi wa 2010 umeiweka CHADEMA kuwa
Kambi rasmi ya upinzani pamoja na sarakasi za Hamad Rashid na Kafulila
ambazo zilishindwa.
Mnaokumbuka
tena katika chaguzi zote ndogo tangia 2005, ni CHADEMA na CCM ndo
vimekuwa na ushindani wa kweli.Mnakumbuka
kiteto,Tarime,Biharamulo,Busanda,Mbeya Vijijini,Igunga,Uzini,na sasa
Arumeru? baadhi ya vyama vimekosa hata pumzi ya kuingia kwenye uchaguzi.
Kwa
hiyo hakuna haja ya kuunganisha vyama vya upinzani kama ilivyokuwa
inasemwa na baadhi ya watu hata wasomi.vyama vinaweza kuungana mkono tu
na siyo kuungana.vilevile hakuna haja ya kuogopa kusajili vyama vipya
kwani hata vikiwa 1000 itabaki kuwa CHADEMA Vs CCM.Kweli tunakoelekea ni
kuzuri
Mdau
No comments:
Post a Comment