Wednesday, February 29, 2012

CHADEMA NA CCM KAMA REPUBLICAN NA DEMOCRATC



Inavyoanza kuonekana kwa sasa vyama hivi pekee ndivyo vitakuwa vikimenyana kwenye chaguzi kubwa.ni kama marekani.Naambiwa kule japo kuna vyama vingi sana vidogo hata vya kikomunisti,lakini nyote mnajua kuwa kwa karne sasa ni Republicans na Democrats pekee wanaotawala hasa siasa za nchi hiyo.Mwenendo ulivyo kwa sasa hapa nchini Ni CHADEMA na CCM. Tangu uchaguzi wa 2005 dalili hizi zilianza kuonekana hasa bungeni ambapo ungedhani kulikuwa na wabunge wa vyama hivyo pekee.japo CUF kiliongoza upinzani bungeni lakini kwa maoni yangu ni wabunge wa CHADEMA wale 11 waliojenga taswira ya upinzani.uchaguzi wa 2010 umeiweka CHADEMA kuwa Kambi rasmi ya upinzani pamoja na sarakasi za Hamad Rashid na Kafulila ambazo zilishindwa.
Mnaokumbuka tena katika chaguzi zote ndogo tangia 2005, ni CHADEMA na CCM ndo vimekuwa na ushindani wa kweli.Mnakumbuka kiteto,Tarime,Biharamulo,Busanda,Mbeya Vijijini,Igunga,Uzini,na sasa Arumeru? baadhi ya vyama vimekosa hata pumzi ya kuingia kwenye uchaguzi.
Kwa hiyo hakuna haja ya kuunganisha vyama vya upinzani kama ilivyokuwa inasemwa na baadhi ya watu hata wasomi.vyama vinaweza kuungana mkono tu na siyo kuungana.vilevile hakuna haja ya kuogopa kusajili vyama vipya kwani hata vikiwa 1000 itabaki kuwa CHADEMA Vs CCM.Kweli tunakoelekea ni kuzuri
Mdau

No comments:

Post a Comment