Waziri Nchimbi amesema “wamekubaliana na kusaini kumaliza tofauti baada ya kufanyika kikao cha mwisho cha upatanishi kati ya Ruge na Mr II ambapo katika upatanishi huo, pande zote mbili ziliridhika kuwa msingi wa mgogoro wao ni kuamini kwamba upande mmoja hauutendei haki upande mwingine”
Waziri Nchimbi amezidi kuamplfy kwamba “kwenye hotuba yangu kwenye bunge lililopita kuhusu vijana Afrika, nilizungumzia haja ya watu kumaliza tofauti zao na kusameheana ambapo baada ya kutoka kwenye mkutano ule Mh Joseph Mbilinyi alikuja kuniona akaniambia muheshimiwa Waziri unajua umeongea mambo ya maana lakini nilitarajia baada ya kusemea pale kwenye kipaza sauti ungekuja kuniambia mimi, haya tuanze huo mchakato wa suluhu, nikamwambia hatujachelewa, bado tunaweza kufanya, nikamuuliza kama ni kweli tufanye mazungumzo ya kuwapatanisha wote wakakubali baada ya kufanya vikao vya kutosha”
Kwa upande wake Ruge Mutahaba amesema “tumepanga mikakati ya jinsi tutakavyokua tunakutana na Mh Sugu kuendelea kusaidia sanaa yetu hii, ni kweli kabisa tumesaini bila shinikizo lolote, tunaamini sasa ni hatua ya kusogea mbele tuachane na yaliyopita”
Mr II alifunga mjadala kwa kuamplfy zaidi kwamba “ni kweli tulikua katika vita na vita lazima ifike mwisho labda iwe ni vita isiyo na malengo ndio haitaki suluhu lakini kama ilikua na malengo ina maana inapopatikana fursa ya suluhu kama kweli ulikua na dhamira a dhati kwa kile unachokipigania lazima ukubali kukaa chini na kutafuta suluhu ili tusonge mbele, tumekubaliana, sasa tunasonga mbele na wengine sasa hivi tupate fursa sasa hivi kujikita zaidi kwenye siasa za kitaifa”
No comments:
Post a Comment